PENZI LANGU 18 - 20 MWISHO

 PENZI LANGU 18 

PENZI LANGU
PENZI LANGU 18


Asubuhi mapema kuli pambazuka na mvua nyepesi na mawingu machache sana Aisha kama kawaid aliamka na kumuandalia nguo mmewake na Kisha akavaa nguo zake za kuzuia baridi na raba zake akatoka nnje na alipotoka akamkuta Dan ameshafika anamsubiria walisalimian Kisha aisha akamuhuliza

"je angekua wakwanza kutoka mmewangu ungemwambiaje?"

"Aisha Mimi simuogopi yeyote yule Kwenye hii familia yko zaidi ya wazazi wako huyo mmewake Hana nguvu kunizidi"

"Sawa tuachen na hayo mambo nadhani tuelekee sehemu husika jabka ya mvua kuanza kunyesha Tena"

basi walianza kukimbia taratibu Hadi kufika Kwenye nyumba hiyo ambayo anaishi Samuel na alipotaka kugonga geti mara simu yake ikaita akatoa Kwenye mfuko na kutazama mpigaji alikua Samuel akaginga geti na Samuel akatoka na kumkuta Aisha akiwa na Dan aliwakaribisha ndani.


Aisha alikua anataka kuzungumza na Samuel pia wakajukuta wanazungumza Kwa pamoja Dan akawambia

"Hamna haja ya kupaniki sawa bwana Samuel Aisha ni mdogo wangu na alinisimukia juu ya kile kilichotokea kati yenu Jana lakini kiti ambacho ukijui ni kimoja tu wewe ni kijana mdogo sana na huwezi kujua Kila kitu ila nataka kukwambia kitu kimoja kuwa Mimi najua Kila kitu kuhusu vifo vya wazazi wako"

"kaka unamaanisha nini kusema hivyo?"

"ndiomaana nilikuambia kua nimekuja hapa kwasababu maalumj hivyo unapaswa uwe mtulivu kwaajiri ya kunisikiliza"

"Sawa kaka nakuskiliza"

"dogo Mimi ni moja ya waliotumiwa kutekeleza hiyo misheni ilikua wauliwe wazazi wa Huyu Binti ila Mimi nikawatafuta watu ambao wangeweza kunusuru maisha ya wazazi wa Aisha ukizingatia ni watu ambao walitaka kufa kwaajiri ya pes ana Mali zao wenyewe,hivyo baada ya kutafuta sana nikakutana na hao unaosema wazazi wako nijaongea nao nikawapa pesa walizohitaji na wakavaa sura za kutengenezwa za wazazi wa Aisha Kisha nikawapeleka sehemu husika lengo la wale jamaa halikua kuuwa ila kilichowafanya wade ni mdomo wa baba Yako maana yeye alikua anajibu Kwa kujiamini na niliwaelekeza kuwa wasiwe wanaongea Chochote lakini baba Yako alikua mkali sana ndio ikapelekea vifo vyao lakini ikisema wazazi wa Aisha nakukatalia Mimi ndio chanzo,lakini pia hao wauwaji wako gerezani sasahivi japokua Kuna baadhi ya watu wapo huru na wanadunda tu lakini hapa nipo Kwenye mchakato wa kuwapoteza Kwenye uso wa dunia mazima"

"kaka kama ni hivyo basi naomba nishirikiane na wewe Kwenye hili"

"na mimi nataka kuripa kisasi Kwa wote wakiotaka kuuwa wazi wangu na hata waliowawa ni kama wazazi wangu na nimeumia pia"

Dan alinyoosha mkono Kwa kuimarisha umoja wao Kisha akafata Samuel na Aisha akamalizia na kusema

"kazi ianze hatutakiwi kuwa wazemne hata kidogo"

baada ya kukubaliana tayari Aisha na dan waliaga na kukubaliana kuanza kazi kwa haraka sana wakati huo Dan anaandaa material yote.

Aisha alipofika nyumbani kwao akaingia ndani na kumwambia Dan

"Dan subir hapo nachukua funguo za gari nikurudishe nyumbani kwako"

Aisha aliingia ndani na kumkuta mmewake hajaondoka akamuhuliza

"baba junior kwani hujaondoka tu,mawazo yangu jilijua umeenda umerudi?"

"umesahau kama Leo napumzika mkewangu?"

"aah nishasahau mwenzio,basi Wacha nikaoge nimpeleke Dani kwao"

"natokea wapi"

"Kuna sehemu alikua ameenda Sasa nimekutana nae hapo njiani wakati narudi nikamwambia nimpe lifti ndioa amekubali"

"ooh Sawa lakini kwanini tusiende Moja Kwa Moja kule kea brother?"

"Suma Yani ukishikiria jmbi basi Sawa jiandaeni"

wakati Aisha anaoga bafuni Suma aliwaogesha watoto Aisha alivyotoka bafuni akawavakisha nguo vizuri na yeye pia Kisha akatoka nao nnje Dan alimchukua maira na kuingia nae kwenyee gari Aisha akamwambia

"kuna sehemu tunaenda hivyo tutakuwahisha kwako ndio tuwende huko"

"Haina shida"

mara Suma alitoka nnje na Kisha akamsalimia dan na kuwaacha gari kuondoka zao.


walifika Kwenye eneo husika na wakashuka garini na kuingia ndani Dan alibaki Kwenye gari hakutaka kuwaingialia mambo Yao.

walisalimiana na kutambulishana Kisha wakapiga story chache Suma akamwambia mkewake kua hao ndio watu ambao alikua anawasikulia kua ndio wamempokea Aisha alifurahi sana na Kisha wakaaga na kutaka kuondoka wote na mkewake walitoka nnje kwaajir ya kuwaaga vizuri maana ujio wao uliwachanngamsha sana na kelele za watoto wao.


lakini Baad ya kutoka nnje wakati wanaagana Dan alishtuka sana na kutikiza kichwa chake kama vile amegundua kitu akalala Kwenye siti Ili asipate kuonekana Kisha Suma na Aisha waliingia Kwenye gari na kuondoka zao huku wakimuomba msamaha Dan Kwa kumchelewesha Dani hakua anajari Wala Nini alikua yupo bize na simu yake.


walimfikisha nyumbani anapoishi na Kisha wakarudi nyumbani kwao Suma akasema

"ila Aisha yule jamaa mi simpendi kabisa yani"

"kwanini Sasa au amekukosea Nini?"

"Sina Imani nae juu Yako naona jinsi anavyokutazama vibaya Hadi naona wivu"

"sum jamani hivi hujui yule nikaka kaka yangu na hawezi kufanya hivyo sababu tumekaa pamoja Kwa muda mwingi na hakuwahi kuniambia Chochote kibayaa ambacho unakiwaza na sasahivi ni zaidi ya mshikaji wangu Wala hata usiwaze vibaya juu yake"

"simpendi kabisa yani ila ndo basi tu tu"

"acha wivu Suma jamani hee"


basi Suma aliingia chumbani kwake akawa anaacheza na wanae huku Aisha alikua anapewa update zote kuhusu yule jamaa Dan alintumia ujumbe na kumwambia

"Aisha yule jamaa sio mtu mzuri kabisa Dio alikua dereva ambae alitumika suala Zima la kutaka kuwauwa wazazi wako ila yeye aliwahi kukimbia ndiomaana hakukamatwa"

"Dan kwahiyo tunafanyaje Sasa?"

"nimempa taarifa Samuel kesho misehni yetu itaanza na wewe hapo sijui udanganye Nini ambacho kitakuweka nnje ya familia Yako Kwa muda kidogo"

"subiri nifanye kitu"

Aisha akifikilia Kwa muda Kisha akapata jibu akamchezea mchezo mmewake akaanza kupiga simu za mara kwa mara na meseji za mapenzi Kisha Aisha alipoingia chumbani akajifanya kushika simu ya mumewake na kumkuta meseji nyingi za mapenzi Aisha akijinunisha sana na kumpa mtihani Suma wa kumbembeleza Aisha kikua amekasirika sana Suma alijitetea sana kwa kitu ambacho hajafanya lakini Aisha alikua hataki kumuelewa hivyo suma akaamua kumwambia

"Sawa Isha kama unaniona Mimi malaya sawa fanya maamzi ambayo unaona ni sahihi fanya Chochote kile"

Aisha akafurahi moyoni japokua alikua anumia kuwa mbali na watoto wake lakini hakua na jinsi kufanya kwaajir ya furaha Yao ya siku zote za maisha Yao.

Aisha alichukua begi na kuweka nguo zake na kuondoka zake,,aliwaacha watoto wakiwa wanalia sana hata Suma pia alishindwa kujizuia maana alihisi maumivu makali sana kuondoka Kwa Aisha bila ya kosa lolote.


basi siku Ile iliishia Kwa Dani wakiwa wote watu Samuel Dan na Aisha.

wakaanz akuoanga mipango Yao na usiku wa siku Ile wakamtumia Aisha kama chambo na kumwambia

"unapaswa uwende pale kuzungumza na yule mwanamke wakati huo sisi tunafanya mpango wa kumteka mmewake Ili tupate kujua mengi kuhusu wao"


Aisha alikubali na akilini mwake tayari alikua na mpango mzima kuhusu huo mchezo wao.


ilikua saa4 usiku Aisha alifika kwenye hiyo nyumba ma kugonga mlango mwanamke alifungua na kumuona Aisha akiwa analia sana baada kumuhuliza akaanza kumsimulia mambo ya uongo kabisa na Kila alipojaribu kutaka kumpigia simu Suma Aisha alimkataza na kumwambia hataki hata kumuona.

lakini wakati ansmzuga Kwa staili hiyo huku Samuel na Dan tayari walifanikiwa kumchukua mwanaume wake na kuondoka zake,Aisha alipopigiwa simu kujulishwa kua mchezo umeenda sawa akajifanya kutabasam na kusema

"waoo dada Suma amepiga simu mwenyew kama nilivyotaka asante Kwa kunipokea Wacha niende"

"eeh mapenzi haya jamani haya usiku mwema Aisha"

Aisha aliondoka na wakati yule mwanamke anaingia ndani alipigwa na kitu kizito sana ambacho kilimfanya aanguke chini kama zigo la viazi...

usikose itaendelea...


PENZI LANGU 19

Baada ya yule mwanamke kuanguka Kwa kupigwa na kitu kizito mara Dan alitoka chumbani akiwa na yule mwanaume Kisha wakaondoka nae.


waienda nae Hadi nyumbani kwa kina Dani wakaanza kumuhoji 


"sema kazi yako kuu na tunataka utuambie watu walipo mtaani na waliogerezani wanamoango Gani?"


"mtaani nimebaki Mimi na mwenzangu ambae nae alihusika kwenye kuchoma moto kwenye msitu ambao alifungwa mtoto wao yeye pia alikimbia na mpaka Sasa sijajua yupo wapi maana hatujabahatika kukutana Tena na waliogerezani walikua wanamoango wa kutoroka na hata hivi karibuni nilikua natimiza mpango kadhaa wa kuwatorosha"


Dan alimtandika sana na kumwambia


"Sasa sikia nitakupa Kila kitu Ili uwatoroshe ila kila unachofanya nitakua nakuona hivyo hata uende wapi Kila kitu nimeandaa kwaajir Yako hivyo ukijfanya ujanja Kila kitu kitakua kibaya kwako sitaki kukuuwa ila utapata mateso makali sana"


"samahani kaka naomba usiniuwe"


"siwezi kukuuwa ila fanya kaka ninavyotaka"


yule mjamaa alikubali na wakikaa nae Kwa siku kadhaa Kisha siku ambayo aliwaahidi kuwa atawatorosha alifika kwenye eneo husika haraka na kuanza haraka to zake katika hizo harakati walifanikiwa kutoroka watatu lakini mmoja aliweza kupigwa risasi na alifariki hapo hapo na wale waliobakia wakawa wanajilaumu sana kwa kumpoteza mwenzao.


yule jamaa aliwapeleka Moja Kwa Moja Kwa Dan sababu alishamchimbia mkwara kuhusu kama atakimbia.


huku njiani aliwambia kuwa amepata chimbo hivyo baada ya kuwafikisha hapo na kuonana na Dani wakimlaimu sana yule ambae amewatirodha na kumtukana sana sio asiah sio Samuel wote walikua na hasira sana juu ya walichowafanyia Aisha alikua anawabana sana sehemu zao za Siri Ili wapitie hata nusu ya maumivu ambayo alikua nayo Kwa kipindi chote baada ya kuambiwa wazazi wake wamefariki upande wa Samuel pia alikua na hasira sana juu yao sababu aliambiwa hao ndio waliowau wazazi wake kitu ambacho hata wao walikataa Dani aliwasimulia ishu nzima ilivyokua walimluamu sana Kisha akawaambia


"nilifanya hivyo sababu ya kuokoa maisha ya mabisi zangu hata mngekua nyie mungemsabanishia matatizo makubwa mtu ambae amekutoa kwenye shida hiyo kitu haipo kabisa ndiomaana nikaamua kuwaokoa Kwa staili hiyo"


Aisha alivyoona anacheleweshwa Kwa maneno mengi alichukua bastora na kuwapigia baskra wawili na kubaki wawili yule jamaa na mmoja wapo ambae ametoka gerezani akaanza kumlaumu yule jamaa


"Sasa mwanangu ndo umekuja kutuuza hivi Bora ningebaki gerezani ningeendelea kula ugali na maharage na kuitumikia nchi yangu Kwa kufanya kazi za kijamii Sasa umeniletea hapaili nitangulue mbinguni sio poa mwanangu nakumaind kinoma Yani na nakuambiaje huu moto ulipuwasha Leo kaa mbali na mimi hata ukiniona huko mbinguni usinisogelee maana nitakufanyia kiti kibaya sana boya wewe"


Aisha Baada ya kuwafyatulia risasi wale wawili alitoka nnje akabaki samule na Dan,Dan alitoa karatasi nyeupe na kumpatia Samuel na kumwambia asisome hapo akasome pindi atakapokua pamoja na Aisha Kisha akampa ruhusa ya kumuuwa mmoja kati ya hao samule alifyatua risasi Kwa mmoja na kumgeukia Dan pia kutaka kumfyatulia risasi lakini Dani aliheuza Kwa yule jamaa na kumfyatulia risasi Kisha akajifyatulia pia na kumwambia samule aondoke eneo Hilo kabla ya polisi kuingilia kati na kumkamata yeye,samuel aliamua kuondoak eneo Hilo Dana alitoa simu yake na kupiga polis na baada ya muda polis walifika kwenye eneo husika na kukuta Dana ameshika karatasi ikiwa na maelezo mafupi na pia alikua amehsuka simu hivyo kiongozi akichukua ile karatasi na kuoka maelezo yote Kisha akasema


"hizi maiti kumbe ndio zile ambazo zimetoloka gerezani na hawa nao pia wanahusika kwenye Vifo vya wazazi wa Binti Aisha,hili ni jambo la kushtukiza kwanini wajiuwe pamoja lazima kuna jambo nyuma yao"




maiti zote zilikusanywa na kuingiwa kwenye gari na kuondoka nazo.




upande wa hotelini Aisha anaonekana akiwana uoga sana juu kile alichokifanya alikua anakunywa sana pombe mara simu yake ikaita Aisha alipokea na kuzungumza


"nani wewe?"


"Aisha Mimi Samuel nataka kukuambia jambo uko wapi?"


"nipo hotelin hapa"


"nielekeze hoteli Gani?"


Aisha alimpa maelekezo sehemu alipo Kisha Samuel alifika Kwa haraka sana na kumkuta Aisha anakunywa pombe kama kichaa Samuel akamwambia


"Aisha kaka Dan ametuachia ujumbe kwenye hii karatasi na amesema nisiisome hii barua mwenyewe nikutane na wewe tusome pamoja"


"ohk soma Samuel nakusikiliza"


"kwenu ndugu zangu wapendwa mimi ni kaka yenu Dan nimeanidka barua hii kwaajir ya kutaka kuwaaminisha kuwa msiwe na wasiwasi najua Sasa mioyo yenu imefurahi Kwa kuripa kisasi ambacho mlikua mnatamani sana kukiripa lakini haya Mimi niameamua kujiuwa sababu nilikua ni Moja wa watu wabaya hasa samule nisamehe sana Kwa kuwalaghai wazi wako na kuwasababishia kifo bila makubaliano kuanzia Sasa ishini Kwa amani na furaha kwasasa Nawapenda sana na hii ibaki kuwa Siri yenu Nawapenda sana"




Samuel baada ya kumaliza kuzima ujumbe huo alijikua anaumia sana na kujihuliza


"inamana aliniondoa Kwa haraka na kujiuwa kabisa nilimzoea Kwa siku chache sana lakini alikua mkarimu sana lakini naomba mungu amoumzishe Kwa amani huko alipo"




haya Aisha pia alikua analia sana baada ya kuskia ujumbe huo.




mpaka inafika asubuhi wakiwa pale pale mara simu ya Aisha ikaita alipomtazama alikua mumewake anampigia simu alipokea na kuanza kulia Suma akamuhuliza


"Aisha mkewangu unalia Nini mbina unanifanyia niwe na wasiwasi mkewangu tatizo Nini?"


"Suma nimekukumbuka sana mpenzi wangu na watoto wetu"


"haya Mimi Aisha wangu umeniachaa na watoto Kila siku wanalia kwaajir Yako simu yangu haukua ukipokea Tena Wala hata kumbe zangu hakuwahi kujibi shida Nini hasa"


"Suma tutakuja kuzungumza nitakaporudi nakupenda sana lakini pia nisamehe sana"


Aisha alikataa simu na kuizima kabisa,Kisha akamwambia Samuel


"Samuel wazazi wangu wapo nnje ya nchi nataka twende Mimi na wewe Ili wakakuombe msamaha najua hawataweza kurudi huku sababu tayari wameshazoea maizngira ya kule hivyo kama utakua tayari naomba tujiandae Kwa safari"


"Samuel hakua na oingamizi na lile suala walijiandaa kisha Aisha aligharamia Kila kitu kuhusu safari yao na kuondoka Tanzania bila ya kumwambia Suma kama anaondoka.




baada ya kufika kwenye nchi husika Aisha alimkaribisha Samuel wakaingia ndani na kumkuta mama yake akiwa anatazama tv Aisha akamshtua mama yake Kwa sauti


"saplaiz...!"


mama yake hakuamini kumuona Aisha akiwa halo alimkumbatia Kwa furaha saña na kumuhuliza


"unaendeleaje mwanangu na huyu mgeni ni nani na watoto wanaendeleaj?"


maswali ya mama yake Aisha yalimua mengi kiasi kwamba Aisha alishindwa ajibu lipi na aliache lipi.


Kabla ya kuanza kutaka kuzungumza mara baba yake na mdogo wake walifika Aisha kama kawaida alimkumbatia baba yake na kumsalimia na mdogo ake pia Kisha wakiwa wamekaa wantaka kuzungumza mara ghafla mlango uligongwa...


je ni polisi ambao walikua wanawashuku Aisha ya samule kua wauwaji au Ninani usikose itaeendelea....


PENZI LANGU 20

Wakiwa wamekaa wantaka kuzungumza mara mlango uligongwa baba yake na Aisha alienda kufungua mlango na Baada ya kufungua akakutana na askari wa hapo nchini akazungumza


"Kuna raia wawili wamingia humu ndani mdamchavhe uliopita hawakufanyiwa uchunguzi kama ni raia kutoka wapi?"


"Samuel na Aisha walitoka na kuonesha vitambulisho vyao Kisha wale polisi wakaondoka baada ya kujiridhisha lakini walidai watakuja Tena kama kunatatizo limetokea baada ya kuondoka baba yake Aisha akahuliza




"Aisha Kuna Nini kimetokea mbina uantaka kutingiza kwenye matatizo shida Nini?"


"baba na mama huyu mnaemuona hapa ni kijana ambae wazazi wake walikua badala yenu nyie hivyo nimemleta kwenu kwaajir ya kumuomba msamaha"


"we mtoto unaongea ujinga Gani?"


"mumewangu nikweli alichokisema Aisha hivi nani anaeweza kujitilea kufa yeye badala yako na walati huusiani nae hata kudogo eeh kumbuka mumewangu hata yeye ni mtoto alitakiwa awe na wazazi wake lakini tumemfanya awe mpweke sana maskini,baba naomba utusamehe sana Kwa kilichotokea najua hatuwezi kuripa Kwa kile ambacho kimetokea lakini kauli ya kudhirisha msamaha huu utatuponya hata wazazi wako pia kama walikua wamechukia watakunjua riho zao kwaajir yetu na kuhitaji tuishi kwa amani bila malumabano"


"mama usijali kuhusu hilo nimewasemehe Kwa moyo mmoja lakini nina ombi Moja kwenu kama mtaliafiki"


"wazo Gani kijana sema tunakusikiliza"


"naomba kama mtamikubaki niwe Moja ya familialia wenu"


mama yake Aisha alitabasamu na kumwambia


"hee Hilo tu Wala hata usijali kijana wangu jusikie amani kabisa"


basi walifurahi pamoja lakini baba yake Aisha alikua bado anahasira akamuhuliza Aisha


"nimekuhuliza Kuna Nini kimetokea Hadi polis waje hapa?"


"baba tumeripa kisasi Kwa walioshiriki kufanya mauwaji na Dan NDIO alifanya yote na hata yeye pia amejiua na kukiri hata yeye amehusika"


baba yake Aisha alichoka sana kwa kile alichokisikia na baada ya muda mfupi polisi walikua Tena na safari hii waliwachukua Samuel na Aisha kwenda kutoa maelezo mafupi na walipoachiwa walati wanarudi samule alikua anafuraha sana kumwambia Aisha


"natamani tusirudi Tanzania kwanini tusiishi huku?"


"hapan Samuel siwezi kuishi huku sababu Tanzania Kuna familia yangu najua kua hata hii ni familia yangu lakini nimeolewa tayari siwezi kuishi na wazazi Tena"


samule alibaki kimyaa tu.




baada ya siku kadhaa Aisha aliaga kua anaindoka na Samuel pia hivyo waliondoka pamoja Tena kama walivyoenda.




Aisha alifika nyumbani kwake na kufungua geti la nyumba Yao akawakuta watoto wake wanacheza na baba yao Kwa furaha saña lakini lilipofunguliwa tu geti wote waligeuka n kutazama getini na wote wakaanza kumkimbikia mama Yao Suma pia alimkimbilia Aisha aliwaacha watoto na kumkumbatia mmewake Kwa furaha saña na mabusu kama yote Suma hakuamini kama Aisha amerudi Tena kwake akamwambia


"siamini kama ungerudi Aisha wangu"


"Suma sikua na sababu maalum ya kuacha Suma naomba nisamehe sana mpenzi wangu"


"I miss you Aisha na naomba tusahau yote yaliyopota na tuanze upya"


Aisha hakutakua Tena kumkumbusha yaliyopota na baada ya kuridhika na mazungumzo yao ya kimahaba wakawabeba watoto wao ka kuingia ndani wakiwa nafuraha.


Aisha akisema


"baada ya Leo nataka twende kwa mama maana tangu aondoke sijawahi kuongea nae"


"hata mimi pia sijawahi kumtafuta"


basi pale walipiga story nyingi Kisha Aisha alipoingia chumbani akakuta mabadiriko sana maana tayari watoto walishatengezewa vitanda vyao Aisha alifurahi sana kwakua watoto walikua wameshalala waliwalaza kwenye vitanda vyao Kisha Aisha akamwambia Suma


"umekua ukinijari siku zote sikua najua kama hata watoto ungeweza kuwajali hivi na wapo wawili na vile wanautundu Suma nakupenda sana"


"Aisha yote nimefanya kwaajir ya kujisafisha kwakonkwa kile nilichokifanyia kipindi Cha nyuma na tukiachana na hayo Sasa Leo siwezi kuacha upumzike sababu nimekumiss saña mkewangu"


Aisha alitabasamu na kumtazama Kwa madeko mmewake na vile Suma hanaga Kona Kona fasta tu wakajikuta kitandani..


siku iliyofata walijiandaa vizuri kisha Aisha alimpigia simu Samuel na Suma alimpigia simu juma na marafiki zake wengine Kisha wakakodi Kosta Hadi anapoishi mama yake.


na ilikua siku ya kuzaliwa mama yake Suma hivyo ilikua furaha sana kwa wote.


siku hiyo walimtambulisha mwamafamilia mpya ambae ni Samuel pia Suma na juma pia walisameheana kuhusu ugomvi wa kumsaidia kaka yake ambae alimsaidia na mwisho Suma akasema.


"nawashukuru sana ndugu zangu Kwa kudhiriana na sisi kuanzia mwamzo wa shuguli Hadi hapa mwisho na kitu kingine pia naomba niwashukuru juma na marafiki zangu wakinarama na wengine pia Kwa kunipokea na kunisapoti Kwa kila njia Sina chakuwarioa zaidi ya kuwatakia mafanikio zaidi na umri mrefu wa kuendelea kufurahia Nawapenda sana"


   **WEMA HULIPWA NA WEMA HATA UBAYA HULIPWA NA WEMA PIA KIKUBWA KUWA NA MOYO WA HURUMA KWA BINADAMU WENZETU SABABU HUWEZI IJUA KESHO YAKO MUNGU HUTOA MITIHANI NA YEYE NDIO HUTUTATURIA PIA KIKUBWA NI IMANI NA MOYO WA MATUMAINI**


                ***MWISHO***

Previous Post Next Post

نموذج الاتصال